Deuteronomy 6:20-25

20 aSiku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mwenyezi Mungu wako alikuagiza wewe?” 21 bMwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu. 22Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote. 23Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo. 24 c Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mwenyezi Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo. 25 dKama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mwenyezi Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”
Copyright information for SwhKC